Kwa
tukio hili, vijana wa mjini wanasema; kimenuka! Hivi karibuni wanawake
watano ambao majina yao hayakuweza kufahamika mara moja walinaswa
usiku mnene wakifanya mapenzi na wanaume wawili kwenye chumba kimoja
kilichopo Mwananyamala jijini Dar.
Watu
hao walinaswa katika oparesheni kabambe iliyoongozwa na Kamanda Mkuu
wa Polisi wa Wilaya ya Kinondoni, OCD Wilbroad Mtafungwa pamoja na
Ofisa wa Oparesheni, Inspekta Jacob Swai.
Katika zoezi hilo, polisi walivamia kambi kuu inayotajwa kusheheni
wanawake wanaojiuza iliyopo Mwananyamala A ambapo ‘wauza sukari’ hao
hutumia vyumba vyao kufanya ufuska huo.
Polisi hao walipofika kwenye chumba kimoja kilichopo eneo hilo,
walikumbana na upinzani mkubwa wa watu waliokuwa ndani na baada ya
kufanikiwa kuufungua mlango, waliwakuta wanawake watano na wanaume
wawili wakiwa kimahaba.
Mbali na hao, polisi walifanikiwa kuwanasa wanawake wengine kwenye
vyumba vyao na baadhi mtaani wakijiuza ambapo walipewa kibano cha hali
ya juu.
Imeelezwa kuwa, wanawake hao wamekuwa na tabia ya kujiuza na wakati
mwingine hukubali kufanya mapenzi na wanaume zaidi ya mmoja, hali
ambayo ni hatari sana.
Mkazi mmoja wa eneo hilo, Husein Juma alisema: “Kwanza tunampongeza
Kamanda Mtafungwa kwa operesheni hii, wanawake hawa wamekuwa ni tatizo
kwani wamekuwa wakijiuza waziwazi na kutupa ovyo kondomu.
Naye Inspekta Swai alisema wamekuwa wakipokea malalamiko kutoka kwa
wananchi wa eneo hilo wakaona ni vyema kuyafanyia kazi ambapo
waliwakamata zaidi ya watu 35, wanawake kwa wanaume wanaohusika.
Home »
mchanganyiko
,
mpya
» WANAWAKE AWATANO WATIWA MBARONI....KISA, WAKUTWA WAKIFANYA UFUSKA NA WANAUME WAWILI KWA PAMOJA
WANAWAKE AWATANO WATIWA MBARONI....KISA, WAKUTWA WAKIFANYA UFUSKA NA WANAUME WAWILI KWA PAMOJA
Written By Unknown on Wednesday, April 24, 2013 | 7:19 AM
Labels:
mchanganyiko,
mpya
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !